Nay wa Mitego na Diamond Wayapeleka Mabishano yao ya Muziki Kwenye Siasa, Soma Vijembe Walivyotupian

Kampeni za uchaguzi zimewatengenisha maswahiba kwenye muziki, Nay wa Mitego na Diamond Platnumz.

Wawili hao waliohit na wimbo wao ‘Muziki Gani’ wapo kwenye kampeni za pande mbili zenye nguvu kwenye uchaguzi wa mwaka huu, Ukawa na CCM.

Na sasa ubishani wao umehamia kwenye siasa.

Kupitia Instagram, Diamond amepost kipande cha video cha show yake ya Zanzibar kwenye kampeni za chama cha mapinduzi na kuandika: Bado wewe tu @naytrueboy kurudi nyumbani….kama nayaona vile yale maselfie yetu na nguo za kijaniblushlaughingsweat_smile #AboutYesterday.”

Nay amemjibu Diamond kwa kuandika:

Nimekataa siendi popote. Wanasema huu ndo muda wa Wasanii kupiga hela ni kweli, ila mi kwangu itakua tofauti kidogo. Mi ni moja kati ya Wasanii wachache wafanya biashara. Ila kwa kipindi iki cha uchaguzi nimeweka pembeni kidogo maswala ya biashara now ni #Harakati huwezi kumnunua mwanaharakati wa kweli coz ata pesa anajua kuitafuta nje ya #Harakati. Uchaguzi ukiisha we leta izo Deal sasa za mamilioni mia tutafanya, ila kwa sasa tunapigania Maslahi ya nchi na kile wanachotaka watanzania Wengi. Naamini #Mabadiliko2015. @diamondplatnumz hujui kusoma, ata picha huoni?! Watanzania wanataka #Mabadiliko2015.”

Share on Google Plus

About EDITOR

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment