DOMOKAYA AFUNGUKA KUHUSU TUZO ZA MZIKI KWA WASANII WA HIP HOP TANZANIA.

Na Mwandishi Wetu.
MANDOJO na DOMOKAYA ni wasanii walioweza kutengeneza namna tofauti ya uwasilishwaji wa mziki wa TANZANIA (BONGO FLAVOUR) kwa matumizi ya 'Guitor' mbali na falsafa iliyopatikana katika kazi sambamba na ustadi ulioonekana kati yao hawa jamaa ambao walishawahi kufanya kazi mbalimbali zilizofanya vizuri ikiwemo 'Nikupe', 'Wanoknok' na 'Dingi'.

Wakati huu watu hawa kila mmoja anaishi nyumbani kwake kutokana na namna mfumo wa maisha ya binadamu ulivyojengwa. Hasa ikiwa ni watu wazima na kuhitaji kuwa na familia na mambo mengine kama hayo, DOMO aliita "KIUTU UZIMA".

Mbali na hilo, 'Mandojo' na 'Domokaya' wanamiliki duka la viatu vya wanawake linalopatikana maeneo ya 'KARIAKOO' karibu na DDC. Pia wanamiliki studio ya mziki inayofahamika kama 'VAKU RECORDS' kama ilivyoelezwa na DOMOKAYA alipokuwa akijibu swali kutoka kwa 'KAD GO' aliyekusudia kufahamu nini mwelekeo wa watu hawa wawili katika masuala ya mziki pamoja na maisha yao siku ya Jumamosi 07 NOV. ndani ya 'NEW MSASANI CLUB - KILINGE'.
  Mandojo akiwa katika duka la viatu. (Picha na Annapita.com) 

Katika kuwaridhisha mashabiki wake alijikuta akijibu swali lililoulizwa juu ya nini mtazamo wake katika msimamo na muelekeo wa mziki wa 'BONGO HIP HOP' ikiwa imeonekana wazi wasanii wa mziki wa 'BONGO FLAVOUR' kupewa nafasi zaidi na kuibuka kidedea katika vinyang'anyilo mbalimbali ndani na nje ya nchi. 

"Sidhani kama mtu akifanya kitu kizuri kitapingwa, ukweli haufichiki na mtu yeyote akifanya kitu kizuri hakipingwi" Alisema.

Mbali na imani hiyo bado aliongeza na kulalamikia mamlaka juu ya namna anavyojishughulisha katika mziki japokuwa mpaka leo hajapata TUZO licha ya kuonekana ni msanii bora Tanzania.
Share on Google Plus

About KWELI EMCEE

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment