Mafanikio ya kipindi cha Radio cha Walinde Watoto katika kupunguza ukatili kwa watoto

Mratibu wa kipindi cha walinde watoto Neema Kimaro akiongea na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya kipindi hicho pembeni yake ni  Mwandaaji wa kipindi cha Walinde Watoto Kimela Billa katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika studio za True Vision  ambao ndio waandaaji wa kipindi hicho chini ya udhamini wa  UNICEF na uratibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano ofisi hizo zipo  Mikocheni, Jijini Dar Es s salaam"
Mwandaaji wa kipindi cha Walinde Watoto Kimela Billa akifafanua jambo kwa waandishi wa habari  kuhusu mafanikio ya kipindi hicho   katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika studio za True Vision  ambao ndio waandaaji wa kipindi hicho chini ya udhamini wa  UNICEF na uratibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano ofisi hizo zipo  Mikocheni, Jijini Dar Es s salaam.
Mwandishi wa habari kutoka kituo cha Luninga EATV David Gumbo akiuliza swali kwa mwandaaji wa kipindi cha Walinde Watoto mapema leo  kuhusu mafanikio ya kipindi hicho   katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika studio za True Vision  ambao ndio waandaaji wa kipindi hicho chini ya udhamini wa  UNICEF na uratibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano ofisi hizo zipo  Mikocheni, Jijini Dar Es s salaam.

Mwandaaji wa kipindi cha Walinde Watoto Kimela Billa akijibu maswali kutoka kwa   waandishi wa habari  kuhusu mafanikio ya kipindi hicho Katikati ni  Mratibu wa kipindi cha walinde watoto Neema Kimaro na kulia kwake ni Mshauri Nasaha Mwandamizi kutoka CSEMA Fatuma Kauramba  katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika studio za True Vision  ambao ndio waandaaji wa kipindi hicho chini ya udhamini wa  UNICEF na uratibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano ofisi hizo zipo  Mikocheni, Jijini Dar Es s salaam.


Waandishi wa habari wakisikiliza makini maelezo ya waaandaji  wa kipindi cha Walinde Watoto mapema leo  katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika studio za True Vision  ambao ndio waandaaji wa kipindi hicho chini ya udhamini wa  UNICEF na uratibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano ofisi hizo zipo  Mikocheni, Jijini Dar Es s salaam.




Na Krantz Mwantepele, Dar es salaam

Kuhusu Kipindi cha Walinde Watoto
Ndugu waandishi wa habari, katika jitihada za kutoa elimu kuhusu maswala ya Ukatili dhidi ya Watoto, UNICEF na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano na True vision production, walianzisha kipindi cha redio cha Walinde Watoto, ambacho kilianza kuruka hewani kupitia redio mbalimbali hapa nchini mwezi Novemba mwaka 2014. Kipindi hiki kinarushwa na redio 19 nchini Tanzania, bara na visiwani, zikiwemo TBC na ZBC.

Malengo ya Kipindi

Malengo ya Kipindi

Ndugu waandishi wa habari, kipindi cha redio cha Walinde Watoto kilianzishwa kwa malengo yafuatayo;


  1. Kutoa elimu juu ya ulinzi kwa watoto, kufuatia ripoti iliyotolewa mwaka 2011 ambayo ilionyesha ukatili dhidi ya watoto ni tatizo kubwa nchini Tanzania
  2. Kutoa fursa kwa jamii kujadili mazingira salama ambayo mtoto anapaswa kuishi mahali popote atakapokuwa iwe ni nyumbani, shuleni na hata barabarani
  3. Kuelimisha jamii kuhusu umuhimu na  mbinu za kuripoti matukio ya ukatili kwa watoto.
Mafanikio ya Kipindi
Ndugu waandishi wa habari, tangu tumeanza kurusha kipindi cha Walinde Watoto tunajivunia mafanikio mengi;

  • Kwanza kabisa ni kwa vituo vya redio vipatavyo 19 kukubali kushiriki kampeni hii kwa kurusha kipindi cha elimu kwa umma bila malipo. Tulianza na redio 14 zikiwemo TBC na ZBC na miezi michache baadaye ziliongezeka redio nyingine 5 baada ya kuvutiwa na maudhui ya kipindi. Kwa ujumla kipindi cha Walinde Watoto kinasikika nchi nzima.

  • Tumefanikiwa pia kutembelea wilaya zaidi ya 12 nchini Tanzania ili kuhakikisha kwamba tunatoa fursa kwa watu mbalimbali wakiwemo wazazi na walezi kupaza sauti zao katika mambo yahusuyo ulinzi kwa watoto. Miongoni mwa wilaya tulizotembelea ni pamoja na Shinyanga, Magu, Musoma, Geita, Kasulu na Kahama. Nyingine ni Kilosa, Kigoma, Kasulu, Kisarawe, Hai na zile za Zanzibar.

  • Ndugu waandishi wa habari tumefanikiwa kutengeneza na kurusha vipindi zaidi ya 60 vikiwemo vipindi maalum kuhusu mada mbalimbali kama vile ukatili wa aina mbalimbali wanaofanyiwa watoto wakikiwa nyumbani, shuleni, na hata barabarani wakienda na kutoka shule, watoto ulemavu wa ngozi ama albino pamoja na watoto wakimbizi. Tumetoa elimu umuhimu wa kutoa taarifa katika ngazi tofauti pamoja na namba maalum ya msaada wa watoto ya 116.


  • Ndugu waandishi wa habari, jukumu la kuwalinda watoto ni letu sote. Kwa kutambua hili tumefanikiwa kufanya mahojiano na viongozi mbalimbali wa serikali, viongozi wa dini, viongozi wa taasisi na mashirika binafsi, wafanyabiashara, wadau mbalimbali, wanaharakati n.k yote ikiwa na lengo la kupata mitazamo tofauti ya wadau hawa muhimu katika maendeleo ya taifa letu.

  • Ndugu waandishi wa habari, wakati wa uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, tulifanikiwa kufanya vipindi maalum vinavyohusu uchaguzi, tuliandaa midahalo iliyowaleta pamoja wananchi na watoto katika meza moja na wagombea wao wa ngazi za ubunge na udiwani, ili wasikilize ajenda za watoto katika uchaguzi mkuu na kuwaeleza ni kwa namna gani wamejipanga kukabiliana na changamoto zinazohusu ulinzi wa watoto.

  • Kama mnavyofahamu swala la kubadili tabia linahitaji nguvu zetu wote na ni mchakato wa muda mrefu, kwa upande wetu, kupitia kipindi hiki cha redio, kwa asilimia kubwa tumefanikiwa kuongeza uelewa wa jamii kuhusu maswala yahusuyo ukatili kwa watoto na namna mbalimbali za kuwalinda watoto. Tunatumaini mtatuunga mkono katika jitihada hizi.

  • Ndugu waandishi wa habari, tulifanikiwa kufungua tovuti maalumu ya www.walindewatoto.org ambayo imekuwa ikirusha vipindi hivi vya watoto. Tumeweza kufungua akaunti katika mitandao ya kijamii ikiwemo Facebook, Twitter na Whatasapp na kwa kupitia mitandao hiyo tumeweza kufikia maelfu ya watu. Pia tumeanzisha namba maalum ya simu ambayo watu wanaweza kupiga na kutoa maoni yao kuhusu vipindi.

  • Ndugu waandishi wa habari, kwa kutambua mchango wa redio katika kupiga vita ukatili dhidi ya watoto, mnamo mwezi Februari mwaka 2015 tuliweza kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari kutoka redio zote washirika wa kipindi hiki. Mafunzo hayo yaliweza kuwajengea uwezo ili waweze kuzungumzia ukatili kwa watoto, namna mbalimbali ya kuwahoji watu ili kuibua changamoto za watoto, na namna ya kufanya jamii ibadilike na kuona matatizo ya watoto ni yetu sote.

  • Kutokana na ubora wa kipindi, wasikilizaji wengi wameongezeka kitendo ambacho kimewashawishi wamiliki wa vituo binafsi kuongeza muda wa kipindi kutoka nusu saa hadi saa nzima na hivyo kupokea maswali na mijadala yahusuyo watoto kutoka katika maeneo yao.

  • Tumefanikiwa pia kuanzisha vikundi vya wasikilizaji kutoka maeneo mbalimbali nchini ambao husikiliza kipindi kila kinaporushwa na kisha kutupa mrejesho wa yale waliyojifunza. Makundi haya husambaza elimu waliyoipata kwa watu wengine wakiwemo ndugu na marafiki zao.


Tunafanyaje kazi?
Kipindi cha Walinde Watoto kinapata maudhui (content??) kwa kuandaa midahalo mbalimbali, mikutano katika vijiji, mahojiano na wadau, kutembelea wilaya na mikoa mbalimbali pamoja na kupitia mitandao ya kijamii.

Tangu tumeanza kurusha kipindi, tumeandaa nyimbo mbili maalum kwa ajili ya kampeni.
Kama motisha kwa wasikilizaji wetu, tunaandaa mashindano mbalimbali ambapo washindi hupata zawadi mfano fulana (Tshirts), redio n.k

Nini malengo yetu?
Ndugu waandishi wa habari, mwezi wa kwanza mwaka huu tumeanza msimu wa pili wa kipindi cha Walinde Watoto. Tunakusudia kufanya yafuatayo;

  • Kushawishi redio mbalimbali nchini zishiriki kampeni na kurusha kipindi cha elimu kwa umma. Tunakusudia kuongeza idadi ya redio kufikia walau 25 ili tuweze kufikia wasikilizaji takribani milioni 24 nchini Tanzania.

  • Kama tunavyofahamu, maswala ya ukatili kwa watoto yanazidi kushika hatamu. Awamu hii itajikita zaidi kwenye kuzungumzia adhabu mbalimbali za watoto zikiwemo vipigo, matusi, manyanyaso, ukatili wa kisaikolojia na nyingine nyingi.

  • Tunakusudia kutumia namba maalum ya simu kutoka UNICEF kufanya utafiti kuhusu usikilizaji wa kipindi hiki ili kupata mrejesho kutoka kwa wasikilizaji

  • Kuendeleza na kuyajengea uwezo makundi ya wasikilizaji wa kipindi katika jamii ‘community listening groups’

  • Kuongeza nguvu katika matumizi ya mitandao ya kijamii ili kufikia watu wengi zaidi pamoja na kutembelea Wilaya nyingine nyingi.
Wito
  • Tunatoa wito kwa serikali na taasisi mbalimbali kuendelea kutoa ushirikiano ili tuweze kuwahabarisha na kuwafikia watanzania wengi zaidi katika kuhamasisha kuwalinda watoto.

  • Tunatoa wito kwa wazazi na walezi kuendelea kuwajali na kuwalinda watoto wao kama njia mojawapo ya kutimiza majukumu yao kama wazazi.

  • Pia tunatoa wito kwa watanzania kwa ujumla kushirikiana kwa karibu na kamati za ulinzi na usalama wa mtoto katika kulisukuma gurudumu hili la ulinzi na usalama kwa mtoto

  • Endapo utaona mtoto anafanyiwa kitendo cha ukatili basi usisite kupiga namba 116 kwa msaada zaidi, namba hii ni bure kabisa.

Redio zinazorusha kipindi cha Walinde Watoto
Zifuatazo ni redio zinazoshirikiana nasi katika kurusha kipindi cha Walinde Watoto:
1.     Radio Faraja- Shinyanga
2.     Radio Huruma- Tanga
3.     Country FM –Iringa
4.     Ice FM- Makambako
5.     Radio Boma Hai- Hai
6.     Zenji FM –Zanzibar
7.     Bomba FM –Zanzibar
8.     Radio Maria- Dar Es Salaam
9.     Radio Quran- Dar Es Salaam
10.  Best FM – Ludewa
11.  Radio Victoria –Musoma
12.  Dodoma FM – Dodoma
13.  Zanzibar Broadcasting Cooperation ZBC- Zanzibar
14.  TBC Taifa- Dar Es Salaam
15.  Radio FADECO- Karagwe
16.  Radio Jamii Kilosa- Kilosa
17.  Radio Kwizera- Ngara
18.  Radio Upland- Njombe
19.  Radio Kitulo- Makete.
Mwisho
Ndugu waandishi wa habari narudia tena kusisitiza, jukumu la kuwalinda watoto ni jukumu letu sote. Vyombo vya habari tuna nafasi kubwa sana ya kufikia watu wengi zaidi, tutumie taaluma yetu kutetea na kulinda haki za watoto.
Asanteni sana kwa kunisikiliza.



Share on Google Plus

About EDITOR

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment