TDX WANGEX (Wangekewa)
TDX WANGEX
maarufu kwa jina hilo ni msanii wa muziki katika miondoko ya HIP HOP
kutoka "KASKAZINI" Arusha, ndani ya Tanzania ambaye kwa muda mrefu
amekuwa akifanya kazi zake jijini DAR ES SALAAM.
Pia
amekuwa akijishughulisha na biashara mbalimbali ikiwemo Kumiliki hisa
kadhaa katika maduka ya simu na hatimaye sasa anamiliki Ofisi yake
ambaye hujihusisha na uuzaji wa simu, promotion na uuzaji wa copy za
mziki na shughuli zinginezo sambamba na hizo inayopatika mtaa wa AGGREY -
KARIAKOO.
Katika namna ya utendaji, TDX ni mmoja kati ya wasanii wanaomiliki Copy za ALBUM
sokoni pamoja na Singles kwa maana ya wimbo mmojammoja kama
ilivyozoeleka hivi sasa kulingana na uwepo wa soko hulia katika mziki
ndani ya Tanzania hali iliyotiwa nguvu zaidi na kukua kwa UTANDAWAZI.
TDX WANGEX atakuwa katika studio za MLIMANI RADIO (106.5 FM) kupitia kipindi cha FLAVOUR ZONE kinachoongozwa na KWELI EMCEE
kuanzia saa NANE KAMILI (1400) mpaka saaa KUMI KAMILI (1600),
akizungumza juu ya kazi yake ya mziki pamoja na changamoto za wazi
hususani katika mauzo ya Album katika DIGITAL ERA pamoja na shughuli
zinginezo sambamba na mziki wake na maisha kwa ujumla.
Toa mchango wako wa mawazo kupitia:
Facebook : KWELI EMCEE
Twitter : kweliemcee
0 comments:
Post a Comment