Tigo yazindua huduma ya kipekee ya Tigo Games

Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Diego Gutierrez akiongea na waalikwa waliohudhuria uzinduzi wa  huduma mpya ya michezo kidijitali ijulikanayo kama Tigo Games jijini Dar Es Salaam jana.Tigo Games ni huduma katika wavuti  ambayo imesheheni  michezo mingi kwa ajili ya wateja wa Tigo wenye simu za Smartphone au Tablet zinazotumia mfumo wa Android ambao wataweza kupata huduma hii kwa kupakua App ya Tigo Games.


Wasanii wakiigiza kama Mazombie katika kunogesha uzinduzi wa TIGO GAMES


Wasanii wakicheza mpira katika uzinduziwa tigo games mapema jana katika ukumbi wa High Spirit Jijini Dar es salaam


Wadau mbalimbaliwakipata taswira mbele ya gari katika RED carpert 




Wasanii wakiwa katika pozi na mfano wa Risasi katika uzinduzi wa TIGO GAMES 


Wadau wakifurahi jambo katika uzinduzi huo


Mtangazaji wa Choice Fm na Mchekeshaji Idris Sultan akiwa live jukwaani kusherehesha uzinduzi wa Tigo Games mapema jana katika ukumbi wa High spirit Jijini Dar es Salaam


Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Diego Gutierrez akifurahi jambo na Ofisa Mkuu wa Biashara wa Tigo, Shavkat Berdiev (kushoto ) wakati wa uzinduzi 




Wasanii wakitumbuiza nyimbo za michael Jackson



Mfanyakazi wa Huawei akielekeza jinsi ya kucheza Games hizo mbalimbali zinazopatikana katika Tigo Games 


Baadhi ya wadau wakipata maelekezo jinsi ya kuingia katika mashindano ya kucheza Games na mshindi kujishindia Zawadi


Waadndishi wa habari wakishindana kucheza Games katika uzinduzi wa Tigo Games jana usiku 


Msanii wa kizazi kipya Benpol akifanyiwa mahojiano na mtangazaji wa clouds tv Perfect baada ya uzinduzi wa tigo games


Wadau mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa Tigo Games mapema jana usiku




Wadau wakipata picha katika sanamu za michezo ya Tigo Games 


Wadau wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa Tigo Games 
Dar es Salaam, Mei 192016- Kampuni ya simu inayoendesha maisha ya kidijitali Tanzania, Tigo, leo imetangaza uzinduzi wa huduma mpya ya michezo kidijitali ijulikanayo kama Tigo Games. Tigo Games ni huduma katika wavuti  ambayo imesheheni  michezo mingi kwa ajili ya wateja wa Tigo wenyeSmartphone au tablet zinazotumia mfumo wa Android ambao wataweza kupata huduma hii kwa kupakuaApp ya Tigo Games. Kwa wateja wenye simu za kawaida zilizo na intaneti watapata huduma hii katika tovuti ya Tigo Games.
 Michezo zaidi ya 800 inapatikana kupitia huduma hii ikiwemo michezo maarufu ambayo ni pamoja na Buddy Man, Cut the Robe, Zombie Run na Tokyo Drift.
 Akizungumza wakati wa uzinduzi  wa huduma hii mpya jijini Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez alisema, “ Huduma hii mpya ya  michezo  inaifanya Tigo kuwa ya kwanza katikamitandao ya simu Tanzania  kutoa jukwaa la michezo linaloweza kutumiwa  na watu wengi ambapo wateja wa Tigo  wanaweza kucheza michezo mbalimbali  kulingana na chaguo lao kwa gharama wanayoimudu. Tigo imejikita kuendelea kusimamia maslahi ya wateja wake kwa kutoa  bidhaa nyingine nyingi  kwa ajili ya manufaa ya kuwa na simu za kisasa.”
 “Tigo sasa ndio inaongoza katika upatikanaji wa huduma ya 4G LTE nchini, na kwa sasa huduma hii inapatikana katika miji mikubwa 12. Tunaamini kwamba wateja wetu watafaidika sana kutokana na intaneti yenye kasi zaidi itakayo wawezesha kupakua na kucheza michezo hii,” alisema Gutierrez.
Tigo Games ni huduma ambayo mteja akichajua kulipia mara moja, ataweza kuchagua michezoaipendayo na kuicheza atakavyo wakati wowote.  Kuna VIP Club ambayo inampa mteja uamuzi wa kujiunga na kifurushi cha siku, wiki na hata mwezi; pia kinamruhusu mteja kupakua michezo bila kikomo.
Mteja ataweza kucheza michezo kwa mda wowote autakao bila makato yeyote. Malipo ya utumiaji wa data kadri mteja anaendelea kucheza ndio yatakayo hitajika. Uzinduzi wa VIP Games Club utakapofanyika, siku 7 za mwanzo wateja wataweza kufurahia huduma bure kwa kutembelea wovuti huu: http://burudani.tigo.co.tz/games

“Kuanzishwa kwa bidhaa hii  kupo kwenye mikakati ya Tigo  ya kuwapatia wateja wake  bidhaa na huduma zilizo na ubora duniani  ambazo  zinawawezesha  kufurahia kwa ujumla maisha ya  kidijitali,” alisema Gutierrez.
Share on Google Plus

About EDITOR

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment