DIAMOND NA DAVIDO Wakutana Tena Laivu Huko South AFRICA...Hichi ndio Kilitokea Baada ya Kuonana


Imekuwa story ambayo kiukweli kwa mtu anayefuatilia muziki haitaji hata kusimuliwa kilichokuwa kinaendelea kwa zaidi ya mwaka mmoja kati ya Davido na Diamond Platnumz ambao ilidaiwa kwamba wameingia kwenye beef au kutoelewana.

Ukaribu wa mastaa hao wawili ulizaliwa baada ya collabo ya My Number One Remix, baadae mambo yakageuka, kukawa na kama uhusiano mbaya na kila kitu kilikuwa kikibebwa na story za mitandaoni hasa Facebook na Instagram, mashabiki kwa upande mwingine huenda ndio waliohusika pia kuifanya ishu kuwa kubwa zaidi.

Davido aliwahi kupost picha ya Bendera ya TZ alafu akaweka alama ya love.. leo Meneja wa Diamond Platnumz, Hamis Taletale aka Babu Tale amepost picha inayowaonesha wakiwa pamoja, Diamond, Davido, na Mameneja wa Daimond, Salam na Babu Tale mwenyewe.

Pia Davido alipost picha akiwa na mastaa wengine pamoja na Diamond Platnumz kama inavyoonekana hapa chini na kuandika with my ni*** na akamention Diamond kwenye Instagram.


Share on Google Plus

About EDITOR

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment