NEW MUSIC VIDEO : EMANUEL AUSTIN FEAT. BEN POL -RUKA JUu


MFAHAMU EMANUEL AUSTIN MTANZANIA MWANAMUZIKI AISHIYE UJERUMANI.

Emanuel  Austin alizaliwa 27.10.1990 Jijini Dar es salaam Tanzania, na ilipofika mwaka 1996  alihamia Ujerumani Kuishi na wazazi wake, Kipaji chake cha kucheza na kuimba kilianza kuonekana mapema.
Akiwa na Miaka mitano Emanuel Austin alianza kuigiza kama anacheza movie pamoja na rafiki zake wa Kiafrika akiwemo Gregory Msuya na Michael Jackson.  Alipofika umri wa Miaka 15 alianza kupenda na kuimba muziki wa Kugani yani ‘Hip hop’
Baadaye alitafuta baadhi ya wenzake ambao aliona wanaweza kuingia studio na kufanya muziki wa Kughani yaani Rap baadhi ya marafiki zake walikuwa ni pamoja na Miguel Amil Matos, Bernado Ernest na Patrick Kitchens ambapo kwa Mara ya kwanza walifanya vizuri.
Mnamo mwaka 2002 wazazi wake na Emanuel walianzisha Mradi mkubwa wa shule kwa ajili ya kufundisha Salsa huko Großkrotzenburg  jirani na  Frankfurt , ambapo yeye binafsi alijifunza Salsa na sasa amekuwa ni mwalimu mzuri wa Mtindo huo. Na kuanzia mwaka 2005 Emanuel  na baba yake wamekuwa wakiendesha programu ya kuwafundisha watoto salsa.
Kipaji cha nyota Mwanamuziki Emanuel Austin kilianza kuonekana wakati ameanza kuimba Lebo ya MarciRecords moja ya sehemu ambayo inawaunganisha wanamuziki mbalimbali na vijana ambao wanavipaji katika sanaa ya Muziki, akiwa huko Emanuel alishinda tuzo ya Msanii anayechipukia ndani ya Mji wa Hanau, Ujerumani  mwaka 2006.
Mwaka 2007 Emanuel alifanya video yake ya kwanza kupitia wimbo wake wa Put your hands up wimbo uliotoka katika album yake ya Put your Hands up, Album hiyo ilitengenezwa na Muandaaji wa Muziki Dj Verde.
Mwaka 2008 Emanuel alifanya ngoma nyengine ambapo alitoa audio pamoja na video , ngoma hiyo ilikwenda kwa jina la Master of the Game, chini ya usimamizi wa mwandaaji wa Muziki Axel Breitung hii ilikuwa ni nyimbo ambayo ilimuongezea umaarufu zaidi na kusikika katika chanel maarufu za Televisheni kama VIVA na MTV.
Kutokana na mafanikio hayo makubwa Emanuel alianza kuandaa matukio mbalimbali ikiwa ni pamoja na matamasha ya muziki , Mwaka 2008 Emanuel aliamua kufungua darasa la mafunzo ambapo ilikuwa ni Shule ya Muziki inayoitwa Tanzschule Weiss iliyopo Offenbach, ambapo wanafundisha Hip hop, Kuwafundisha watoto kucheza na Salsa Cubana na anampango wa kuanzisha shule ya Muziki Nchini Tanzania.
Kwa sasa Emanuel Austin anafanya kazi katika moja ya shule kubwa ya Muziki wa Dance nchini  Ujerumani  ambapo wachezaji maarufu wa Dance kama Don Omar wapo humo , hata hivyo Emanuel huja nyumbani Tanzania kila mwaka  na sasa Amekuja na ngoma mpya ambayo amemshirikisha Ben Pol inaitwa ruka juu.

Kufahamu zaidi juu ya Emanuel Austin   Mfuate hapa
.
www.instagram.com/emanuelaustinofficial 
www.facebook.com/emanuelaustin 
YouTube : Emanuel Austin 
Twitter: emanuelaustin27 

www.twitter.com/emanuelaustin27
Share on Google Plus

About EDITOR

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment