Idris Sultan akanusha kuwahi kutoka kimapenzi na Wema Sepetu


Mshindi wa BBA 2014, Idris Sultan amekanusha kuwahi kutoka kimapenzi na Wema Sepetu baada ya kuonekana kuwa karibu zaidi katika miezi kadhaa iliyopita.

Akizungumza jana kwenye kipindi cha Mkasi TV kinachorushwa kupitia kituo cha runinga cha EATV, Idris alisema hajawahi kutoka kimapenzi na Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 kama watu wanavyosema.

“Kwahiyo mimi nikiwa natembea na Wema haimaanishi kuna kitu chochote kinaendelea, rumors has nothing,” alisema Idris.

Pia Idris alieleza anawezaje kuwa karibu na Ommy Dimpoz, Diamond pamoja na Wema Sepetu wakati wasanii hao hawaelewani. “Kiukweli ni ngumu lakini hawa ni watu ambao mimi nawahitaji kwenye maisha yangu bila kujali sijui kama wao wananihitaji, ni watu ambao walininspire,” alisisitiza.
Share on Google Plus

About EDITOR

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment