Zitto Kabwe amvisha pete mchumba wake huyu

Kambi maarufu mjini ya Ukapera inatarajia kupata pigo la mwaka pale member wake mahiri na wa muda mrefu, mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe atakapoigika kibuti rasmi.

Zitto amemchumbia msichana mrembo anayetarajia kumbadilisha jina soon kuwa ‘Mrs Kabwe.’

Picha za mbumbe huyo akimvisha pete msichana huyo mbele ya ndugu na jamaa zimesambaa mtandaoni wiki hii.

Kuna picha moja inayoonesha kuwa ni post ya Instagram aliyoiweka Zitto ambapo aliandika: So Beautifu and full of love. I love you.

Kabla ya kufutwa post hiyo ilikuwa imefikisha comments 216 na likes 3,257. 



Share on Google Plus

About EDITOR

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment