Jana katika dimba la Michigani huko Marekani , miamba miwili ya soka ulimwenguni ilivaana. Manchester United wakiongozwa na kocha Van Gaal waliirarua Real Madrid iliyo chini ya kocha Anceloti kwa jumla ya magoli 3-1.
Magoli ya Man U yalifungwa na Ashley Young ambaye aliingia nyavuni mara mbili na Javier Henerndez (Chicharito), huku goli la kufutia machozi la Real Madrid likiwekwa kimiani na Gareth Bale kwa mkwaju wa penati. Ushindi huo umeipa nafasi Man U kucheza fainali ya michuano ya kombe la Mabingwa wa Kimataifa (International Champions Cup) ambapo watavaana na Liverpool
Nimekuwekea video ya magoli yote hapa, ili mdau wangu ujionee mwenyewe:
0 comments:
Post a Comment